Rais
Jakaya Kikwete akizungumza na wakuu wa mikoa,
makatibu tawala na wakuu wa wilaya katika ukumbi wa
St.Gaspar Mjini Dodoma. (Picha na Freddy Maro)
Rais Kikwete amewataka viongozi hao wa Serikali wasiingilie maamuzi yanayotolewa na Mahakama.
“Wako wanaokuja mpaka
kwangu wanasema haiwezekani wewe ni Rais
tusaidie, ukikataa wanasema kwanini uwe
Rais wakati hutusaidii, wanajua ukiwa Rais unaamua kesi unavyotaka kumbe sina mamlaka hayo,” alisema Rais Kikwete.
Amesema, Serikali inaendeshwa kwa kuzingatia sheria la sivyo itaendesha mambo ya hovyo
na kwa ubabe na watu wataichukia na
kufanya vurugu.
Amewahimiza viongozi hao kwenda kusimamia
kilimo na kuweka utaratibu wa kusikiliza matatizo ya wananchi na kuwa na
haraka ya kutimiza wajibu.
“Watu
wanaandika barua hazijibiwi wanaambiwa njoo kesho jambo likikushinda mpelekee
anayehusika kwani kuchelewesha kutoa maamuzi ni kuwanyima watu haki zao.
Amewataka kutambua vikwazo vya maendeleo na kutengeneza malengo mikakati
na hata kama hakuna vikwazo kuwe na maboresho.
Amewataka
kutambua wajibu wa kushirikisha wananchi kwa kuangalia changamoto za maendeleo zilizopo na kuzipatia ufumbuzi ikiwa ni pamoja na kuwatembelea
wananchi na kujua shida yao.
Aliwataka pia kuheshimu mawazo ya watu
watakaowakuta na kutopuuza mawazo yao na kubakia wakitoa amri tu.
No comments:
Post a Comment