Elizabeth Michael 'Lulu' akiwasili katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kwa ajili ya kusikilizwa kwa shauri la ufafanuzi kuhusu wake.
Lulu
anakabiliwa na mashitaka ya kusababisha kifo cha aliyekuwa mcheza filamu
nyota nchini Steven Charles Kanumba aliyekufa usiku wa kuamkia Aprili 7 mwaka huu Sinza Vatican Jijini Dar es Salaam.
Picha zote kwa hisani ya blog ya Francis Dande
Lulu akiwa mahakamani jana
MAWAKILI wa Serikali katika kesi ya mauaji
inayomkabili mwigizaji wa filamu, Elizabeth Michael ‘Lulu’, wamepinga maombi ya kuuchunguza umri wa mshitakiwa huyo.
Mawakili wanaomtetea Lulu wameiomba Mahakama Kuu
ichunguze umri wa msanii huyo au kuiamuru Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam
ifanye hivyo.
Wakili wa Serikali, Shadrack Kimaro ameiomba Mahakama hiyo isisikilize maombi
ya Lulu kwa madai kwamba yaliwasilishwa mahakamani hapo kimakosa, na pia
sheria iliyotumika ina kasoro.
Sheria
iliyotumiwa na mawakili wa utetezi ni Sheria ya Mtoto ya mwaka 2009, kifungu
cha 113 inayoruhusu Mahakama kufanya uchunguzi wa umri wa mshitakiwa.
Kimaro
amedai kuwa, maombi hayo yalikwishatolewa
katika Mahakama ya Kisutu na ‘kugonga mwamba’ na kuongeza kuwa mawakili
wa utetezi walitakiwa kuukatia rufaa uamuzi huo au kuomba mapitio yake, lakini
si kuwasilisha maombi mapya.
Kimaro aliyekuwa akisaidiwa na Wakili wa Serikali, Elizabeth Kaganda,
alidai kuwa maombi ya pili kwa Mahakama hiyo ya kusitisha kesi ya Kisutu ni
batili.
Alidai
ubatili huo ni kwa sababu kesi ya Lulu Kisutu haisikilizwi, iko katika hatua ya
uchunguzi na sheria inataka kesi kusimama ikiwa katika hatua ya kusikilizwa.
Mawakili wa Lulu, Peter Kibatala, Fulgence Masawe na Kennedy Fungamtama
na Kamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (CHRAGG) Joaquine De-
Melo aliyetambulishwa kama mtazamaji, walipinga.
Mawakili
hao walidai kuwa waliwasilisha maombi yao mahakamani hapo kutokana na uamuzi wa
Mahakama ya Kisutu uliotamka kama kuna maombi yoyote yawasilishwe katika
Mahakama hiyo.
Walidai
kuwa Mahakama ya Kisutu ina uwezo wa kutoa uamuzi wa maombi yao kwa mujibu wa
sheria na hakuna walipokosea na kuiomba Mahakama ipuuze maombi ya mawakili wa
Serikali.
No comments:
Post a Comment