Wednesday, April 29, 2009

Milipuko Dar es Salaam

KUNA sauti kubwa za milipuko zinazodaiwa kusababishwa na kulipuka mabomu katika kambi ya jeshi iliyopo Mbagala, Dar es Salaam.
Inadaiwa kuwa ghala la kuhifadhia silaha katika kambi hiyo limelipuka.
Nimezungumza na mkazi wa huko amesema wananchi wamezikimbia nyumba zao, wapo barabarani hawafahamu cha kufanya na wengine wanalia.
Mwanzo kulikuwa na taarifa kwamba ni mazoezi ya jeshi lakini baadaye zilipatikana taarifa kuwa si mazoezi, ni ajali katika kambi hiyo, mabomu yanalipuka.
Inadaiwa kuwa kuna nyumba zimeanguka na huenda kutakuwa na maafa.
Vishindo vya milipuko hiyo vinasikika hadi katikati ya jiji la Dar es Saaam.

1 comment: