Wednesday, April 29, 2009

Wizara yaomba wanaume wafanyiwe tohara

WIZARA ya Afya na Ustawi wa Jamii imesema wanaume ambao hawajatahiriwa watumie busara, wafanyiwe tohara ili kupunguza maambukizi ya UKIMWI.
Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Dk Aisha Kigoda ametoa ombi hilo muda mfupi uliopita bungeni mjini Dodoma.
Matokeo ya tafiti za kisayansi yamebainisha kwamba uwezekano wa mwanaume aliyetahiriwa kuambukizwa Virusi vinavyosababisha upungufu wa kinga mwilini (VVU) ni mdogo kulinganisha na ambao hawajafanyiwa tendo hilo.

No comments:

Post a Comment