Wednesday, April 29, 2009

Breaking News

KAMANDA wa polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, amewataka wananchi wasiende Mbagala kwa kuwa eneo hilo ni hatari kwa sasa.
Kamanda huyo pia kawataka wananchi walioko huko wasikuanyike, na wazime simu zao za mkononi.
Kova amesema, mabomu mengi yamelipuka katika kambi ya jeshi iliyopo Mbagala Kizuiani na hajui chanzo cha ajali hiyo.
Taarifa kutoka eneo la tukio zimebainisha kwamba, moshi umetanda eneo hilo , kuna giza, na pia nyumba kadhaa zinaungua.
Milipuko mikubwa ilisikika saa kadhaa zilizopita, na kuna majengo katikati ya jiji la Dar es Salaam yameathirika.

1 comment: