Thursday, April 30, 2009

JK kuongoza mkutano kujadili mabomu

RAIS Jakaya Kikwete mchana huu ataongoza mkutano wa viongozi wa Serikali kujadili na kutathimi milipuko ya mabomu katika ghala la kuhifadhia silaha mkoani Dar es salaam.
Mabomu hayo yalilipuka jana katika ghala hilo la Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ) lililopo Mbagala wilayani Temeke.
Muda mfupi uliopita Waziri mkuu, Mizengo Pinda amesema bungeni kwamba, baada ya mkutano huo Serikali itatoa tamko kuhusu milipuko hiyo iliyosabisha hasara ya mali, vilema, majeraha, na vifo.

No comments:

Post a Comment