Thursday, April 30, 2009

Cheyo Mbunge Bunge la Afrika




Bunge la Tanzania limemchagua Mbunge wa Bariadi(UDP), John Momose Cheyo kuwa Mbunge katika Bunge la Afrika.

Cheyo kachaguliwa muda mfupi uliopita katika mkutano wa 15 wa Bunge utaomalizika muda mfupi ujao mjini Dodoma.

Wabunge 205 walipiga kura, mbili ziliharibika, Cheyo amepata kura 111, mpinzani wake, Khalifa Suleiman Khalifa amepata kura 92.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda yupo anahutubia Bunge kuhitimisha mkutano huo.

Wabunge walikutana kwa siku 10, waliuliza maswali 108, Pinda aliulizwa maswali 18 ya papo hapo.

No comments:

Post a Comment