Thursday, March 13, 2014

Sitta: Sitapendelea, nitakuwa mtetezi

 
 Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa akimpongeza Samuel Sitta baada ya kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Bunge la Katiba

“Jamani kunichagua mimi ni kama kumrejesha chura kwenye dimbwi la maji alilolizoea. Msiwe na wasiwasi ataogelea tu na ninawaahidi kuwa ikiwa kwa kudra za Mwenyezi Mungu, mtanichagua nitawatumikia kwa uaminifu, sitakubali upendeleo wa aina yoyote, nitasimamia kanuni tulizozipitisha hapa,” 

 “Nitawaongoza kwa utumishi uliotukuka na uadilifu ili tupate Katiba bora, yenye viwango na kwa wakati. Nina hulka ya kuwapenda wale ninaowaongoza, kwa hiyo nitakuwa mtetezi wa shughuli mbalimbali…Ninawaahidi Watanzania kutenda haki na kuwapatia Katiba yenye viwango na kwa wakati.

Mwenyekiti wa Bunge la Katiba, Samuel Sitta

No comments:

Post a Comment