DADA wa
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Grace Mbowe,
wakati anajiunga na Chama Cha Mapinduzi ( CCM) akitoka Chadema. Baada ya kukabidhi kadi ya Chadema katika ofisi za CCM Wilaya ya
Hai Grace alisema.
“Nimeamua
kwa hiyari yangu mwenyewe bila kushawishiwa na mtu, ndio maana nimetoka
Dar es Salaam kuja Hai kwa ajili ya kurejesha kadi ya CHADEMA na
kujiunga na CCM, suala la itikadi lisihusishe masuala ya kifamilia kwani
upendo wetu upo palepale,”alisema Mbowe.

Katibu wa Chama Cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro, Hassan Mtenga akimkabidhi , Grace Mbowe, kadi ya CCM.

Katibu wa Chama Cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro, Hassan Mtenga akimkabidhi , Grace Mbowe, kadi ya CCM.
“Kuwapo kwangu
CHADEMA siyo kwa sababu ya familia, hivyo hakuna wa kunizuia, natoka
kwa utashi wangu, na tutaendelea kuheshimiana na mdogo wangu Freeman
Mbowe katika masuala ya kifamilia.”
“Freeman Mbowe ni mdogo wangu wa kuzaliwa kabisa, hakunishawishi kuingia CHADEMA, hivyo sioni haja ya kuendelea kubaki huku wakati sioni jambo jipya, mimi tangu naifahamu CCM iko vile vile, bali propaganda za upinzani ndizo zinawalaghai wananchi,” alisema.
“Freeman Mbowe ni mdogo wangu wa kuzaliwa kabisa, hakunishawishi kuingia CHADEMA, hivyo sioni haja ya kuendelea kubaki huku wakati sioni jambo jipya, mimi tangu naifahamu CCM iko vile vile, bali propaganda za upinzani ndizo zinawalaghai wananchi,” alisema.
No comments:
Post a Comment