Wednesday, August 29, 2012

Askofu Kanisa Katoliki afariki dunia

Askofu Paschal William Kikoti wa Kanisa Katoliki Jimbo la Mpanda amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika Hospitali ya Rufaa Bugando jijini Mwanza alikokuwa amelazwa.
 
Makamu wa Askofu wa Jimbo la Mpanda, Padri Patrick Kasomo amekaririwa akisema, kifo cha Askofu Kikoti kimetokana na ugonjwa wa shinikizo la damu.
 
Kwa mujibu wa Padri Kasomo, mwili wake utawasili kesho Alhamisi kwa taratibu za mazishi.
 
Padri Kasomo amesema, mwili wa Askofu Kikoki unatarajiwa kuzikwa Jumamosi wiki hii kwenye Kanisa Kuu la Mtakatifu Maria mjini Mpanda.

No comments:

Post a Comment