Thursday, May 17, 2012

Uzembe wa dereva wasababisha ajali, wanne waumia

WATU wanne wamelazwa katika Hospitali ya Mkoa Singida, baada ya basi la Mohamed Trans, kugongana na basi dogo jana (Jumatano) mjini Singida.
Kamanda wa Polisi mkoa Singida, Celina Kaluba, amesema chanzo cha ajali ni uzembe wa dereva basi la Mohamed Trans, aliyetaka kuingia katika barabara kuu ya Mwanza- Dodoma, bila kuchukua tahadhari yoyote. 
Waliojeruhiwa ni dereva wa basi dogo na abiria wake, dereva wa basi la Mohamed Trans lenye namba za usajili, T 848 BEQ alitoroka.
Majeruhi waliolazwa ni Yesaya Samson (dereva wa basi dogo) aliyevunjika miguu yote, Paulo Rajabu, Parick Stephano na William Richard, waliopata majeraha sehemu mbalimbali za miili yao.
Abiria zaidi ya 50 waliokuwa kwenye basi la Mohamed Trans hawakupata madhara.
Basi la Mohamed Trans lilikuwa likitoka Morogoro kwenda Mwanza, basi dogo lenye namba za usajili T 499 BRS Dyana, lilikuwa likitoka Singida mjini kwenda kijiji cha Iglansoni, Singida vijijini.

No comments:

Post a Comment