Tuesday, November 22, 2011

Wanafunzi 6 UDSM wafa ajalini

Chikondi Chasowa- Mmalawi

Nshaija Muganyizi- Mtanzania


Mubiru Patrick- Mganda










Kassim Dadi- Mtanzania



Josephine Kaleso-Mmalawi






Chimuka Hamajata- Mzambia



WANAFUNZI sita waliokuwa wakisoma Shahada ya Uzamili, Hisabati katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ni miongoni mwa watu 18 waliokufa Jumamosi katika ajali ya basi la Taqwa lililogongana na lori mkoani Kagera.

Kwa mujibu wa Makamu wa Mkuu wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, Profesa Rwekaza Mukandala, marehemu hao ni miongoni mwa wanafunzi 10 wa UDSM waliokuwa wakienda Kigali nchini Rwanda kwa ajili ya ziara ya kimasomo katika Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Kigali.

Kwa mujibu wa taarifa ya Profesa Mukandala kwa vyombo vya habari, wanafunzi waliokuwa katika safari hiyo ni wa kimataifa waliokuwa wakisoma shahada ya uzamili kupitia Programu ya Hisabati katika Vyuo Vikuu vya Afrika Mashariki.

Miongoni mwa waliokufa katika ajali hiyo, wawili ni raia wa Malawi, Watanzania wawili, Mganda na Mzambia.

Watanzania waliokufa ni Nshaija Muganyizi, na Kassim Dadi, Wamalawi ni Chikondi Chasowa na Josephine Kaleso, Mganda ni Mubiru Patrick na Mzambia ni Chimuka Hamajata.


Basi la Taqwa lenye namba za usajili T 635 ABC aina ya Nissan Diesel lililokuwa likitoka Dar es Salaam kwenda Bujumbura Burundi liligongana na lori la Kampuni ya Bakhresa lenye namba za usajili RAB 255ACT lililokuwa likitoka Ngara kwenda Dar es Salaam.

Magari hayo yaligongana Jumamosi saa nne asubuhi katika eneo la Lusahunga wilayani Biharamulo.

No comments:

Post a Comment