Monday, October 25, 2010

Man City cha mtoto kwa Arsenal

Raha ya bao

Nasri akifunga bao la kwanza la 'The Underdogs', Arsenal.

Kipa wa Man City, Joe Hart akiokoa penati iliyopigwa na Fabregas.

Fabregas akichezewa ndivyo sivyo

Refa akimuonesha Boyata kadi nyekundu baada ya kumuangusha Chamack wakati akijiandaa kucheka na nyavu. Kiungo mshambuliaji, a.k.a Fab, a.k.a Mtafutie, Cesc Fabregas alipiga penati hiyo, kipa Joe Hart aliokoa.

Boyata akimkwatua Chamack.
BILA shaka hakuna aliyetarajia matokeo ya mpambano wa jana kati ya Arsenal na Man City lakini kilichotokea ndiyo soka.
Si kazi rahisi kuifunga Man City mabao 3-0 kwenye uwanja wao wa nyumbani lakini ukicheza na timu kama ARSENAL, inawezekana!
Msiwalaumu Man City kwa kucheza walivyocheza jana, hawakuwa na namna, ilibidi wacheze hivyo, wanastahili pole.
Kwa tathimini rahisi, Man City walizidiwa, waliteswa, waliumia kwao, na kwa bahati mbaya, wapendwa wao wameshuhudia mateso hayo.
Poleni Man City, hongera Arsenal!

No comments:

Post a Comment