Friday, October 23, 2009

Machozi ya damu

MWANAMKE nchini India, Rashida Khatoon, amekuwa gumzo nchini humo kutokana na hali yake ya kutoa machozi ya damu kila anapolia.

Rashida amewashangaza hata madaktari kwa hali yake hiyo ya kutiririka machozi ya damu kila anapolia.

Kwa siku mwanamke huyo humwaga chozi la damu mara kadhaa.

"Sisikii maumivu yoyote, badala ya machozi ya kawaida, damu zinapotitirika ni kitu cha kushangaza" alisema mwanamke huyo.


Viongozi wa dini wa India wanadai kwamba mwanamke huyo ni miujiza toka Mungu.

No comments:

Post a Comment