Tuesday, April 21, 2009

Tiba ya moyo


Mgonjwa: Daktari naumwa sana moyo.

Daktari: Wewe ni mpenzi wa timu gani ya mpira wa miguu?

Mgonjwa: Kwa Tanzania mimi ni shabiki wa Simba na Ulaya mimi ni mpenzi wa Manchester United.

Daktari: Na unafanya kazi wapi?

Mgonjwa: Nilikuwa nafanya kampuni ya GTV, baada ya kufa nikapata kazi Paradise Hotel Bagamoyo.

Daktari: Una akiba yoyote ya fedha benki?

Mgonjwa: Ndiyo, akiba yangu yote ya fedha ipo DECI.

Daktari: Mmmh, unaishi wapi?

Mgonjwa: Naishi Kwembe wilayani Kinondoni.

Daktari: Duh, subiri kufa maana hakuna tiba mbadala ya maradhi yako.

No comments:

Post a Comment