WATOTO wanne pacha waliozaliwa usiku wa kuamkia Mwaka mpya wa 2014
katika Hospitali ya Wazazi ya META jijini Mbeya wanaendelea vizuri.
Mama mzazi wa watot hao, Aida Nakawala (25) mkazi wa kijiji
cha Chiwanda, Wilaya ya Momba, Mkoa wa Mbeya, amewashukuru wasamaria
wema kwa kuendelea kutoa misaada iliyosaidia watoto hao kukua vizuri.
Baba Mzazi wa
watoto hao, Webson Simkanga (28) amesema, hana uwezo kiuchumi lakini
kutokana misaada mbali mbali aipatayo kutoka kwa wasamaria wema afya ya watoto wake inaimarika.
Simkanga ametoa majina kwa watoto hao wanaotarajiwa kubatizwa Machi tisa mwaka huu katika kanisa la African Mission Church (AMC).
Aliwataja majina watoto hao kuanzia wa
kwanza hadi wa Mwisho kuwa ni Alinikumbu (mtoto mwenye huruma), Daudi, Asifiwe na Anania.
Kwa hisani ya Blog ya Mbeyayetu.
No comments:
Post a Comment