
Wachezaji
wa Liverpool wakishangilia bao la Daniel Sturridge lililoipa ushindi wa
1-0 dhidi ya Manchester United kwenye Uwanja wa Anfield. Huo ni ushindi
wa tatu mfululizo kwa Liverpool tangu kuanza kwa msimu, matokeo
iliyowahi kupata miaka 19 iliyopita. (Picha kwa Hisani ya Gazeti la
Daily Mail la Uingereza)

Sturridge
akishangilia bao pekee la Liverpool, alilofunga leo. Ushindi huo
umekuja wakati ambao mshambuliaji huyu anaadhimisha miaka 24 ya kuzaliwa
kwake leo Septemba 1.

Sturridge
akidondoka baada ya kupiga kichwa kufunga bao hilo akiunganisha pasi ya
kichwa ya Daniel Agger aliyeunganisha kona ya Steven Gerrard.


Sturridge akikumbatiana na kocha wa Liverpool Brendan Rodgers baada ya kuifungia timu yake bao la ushindi.

Steven Gerrard wa Liverpool, akitunishiana msuli na Robin van Persie wa Man United wakati wa mechi hiyo.

Martin
Skrtel (37), akiruka juu kuwania kupiga mpira wa kichwa kuondoa hatari langoni mwa
Liverpool.

Steven Gerrard akipiga adhabu ndogo.
No comments:
Post a Comment