Thursday, August 29, 2013

Askofu Moses Kulola afariki dunia



Askofu Mkuu wa kanisa la Evangelistic Assemblies God Tanzania, Moses Kulola amefariki dunia leo jijini Dar es Salaam.
moses_b8f0d.jpg
Kwa mujibu wa taarifa hizo, Askofu Kulola ameaga dunia katika hospitali ya AMI (African Medical Investments) iliyopo Slipway, Dar es Salaam.
ASKOFU MOSES KULOLA (katikati) AKIWA NA WAIMBAJI WA MUZIKI WA INJILI FAUSTINE MUNISHI NA EMMANUEL MWASOTA NA HAPA ILIKUWA NI MWANZONI MWA MIAKA YA 1970.
ASKOFU MKUU MOSES KULOLA

Askofu Kulola, ambaye amezaliwa mwaka 1928, amekuwa akisumbuliwa na maradhi kwa muda mrefu na kuna wakati alipelekwa India kwa matibabu.

Mmoja wa watu wa karibu wa familia ya Askofu huyo amesema, kiongozi huyo wa Kanisa alikuwa anasumbuliwa na maradhi ya moyo, mapafu na ini.

Askofu Moses Kulola akiwa Israel





No comments:

Post a Comment