JAMES
Lutwe (43) mkazi wa Bunju 'B' katika Manispaa ya Kinondoni Dar es Salaam
anaomba msaada wa Sh 400,000 ili afanyiwe upasuaji wa nyonga iliyovunjika baada
ya kuangukiwa na kifusi.
Akizungumza
na gazeti hili Dar es Salaam jana, mkazi huyo ambaye kwa sasa anatembelea
magongo, alisema alitakiwa kufanyiwa operesheni tangu Julai mwaka jana
alipopata ajali, lakini ilishindikana kutokana na kukosa fedha.
Kwa
mujibu wake, matibabu yote yanagharimu Sh milioni 10.3 lakini kutokana
na ukweli alioueleza kuwa hana ndugu au jamaa mwenye uwezo wa kuzilipa,
madaktari wanaomshughulikia katika Taasisi ya Mifupa (MOI) walimwelewa na
wametafuta namna ya kumsaidia hivyo kaambiwa atafute Sh 400,000.
"Naomba
msaada kutoka kwa yeyote atakayeguswa na tatizo langu kwa sababu ninapata
maumivu makali na hakuna kazi ninayoweza kuifanya kwa sasa.
Fedha zitanifikia
zikitumwa kupitia namba hizi za simu; 0762879490 na 0656214438".
Lutwe
alipata ajali hiyo katika eneo la Mto Mpiji alipokuwa akijaza mchanga wa kuuza
kwenye malori.
Chanzo: HabariLEO
No comments:
Post a Comment