Friday, May 17, 2013

Wanafunzi UDSM, CBE, VETA washitakiwa kwa ukahaba

WANAFUNZI wa kike wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) na Chuo cha Mamlaka ya Elimu na Ufundi Stadi (VETA), Dar es Salaam, wamefikishwa katika Mahakama ya Jiji Samora, wakidaiwa kufanya biashara ya kuuza miili yao. 
 
Washtakiwa hao walikamatwa katika eneo la Kona Baa Ambiance, Sinza wilayani Kinondoni ambao ni miongoni mwa wanawake 35 wanaodaiwa kufanya biashara hiyo na wote walifikishwa mahakamani hapo.
 
Kesi hiyo ilikuwa chini ya Hakimu Willian Mtaki ambapo Mwendesha Mashtaka,
. John Kijumbe, alisema wasichana hao walikamatwa katika mazingira tofauti tofauti.

Wanafunzi hao ni Yasinta Kilimo mwenye miaka 21 (CBE), mkazi wa Upanga, Morin Masatu miaka 19 (UDSM), mkazi wa Kinondoni na mwanafunzi wa VETA, aliyefahamika kwa jina moja la Khadija. 
 
“Nilikwenda pale baa kuchukua simu yangu ambayo ilipotea hivyo waliniita nikaichukue ndipo askari wa jiji wakanikamata,” alisema Khadija wakati akijitetea. 
 
Kwa mujibu wa Bw. Kijumbe, washtakiwa hao wamekosa dhamana baada ya kushindwa kutimiza masharti ya kila mmoja kuwa na wadhamini wawili au kulipa faini sh. 200,000. 
 
Kesi hiyo inatarajiwa kusikilizwa tena Mei 28 mwaka huu, ambapo washtakiwa wote walipelekwa Segerea.

No comments:

Post a Comment