Kuna madai kuwa, kuna wabunge wawili katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wamejazwa mimba na wabunge wenzao.
Awali,
kulikuwa na uvumi kuwa mmoja wa wabunge wa upinzani (Viti Maalum),
akitoka Kanda ya Kaskazini, amepewa ujauzito na mheshimiwa mwingine
ambaye ni kiongozi anayeshika nafasi za juu kwenye moja ya vyama vikuu
vya upinzani nchini (wote majina yao tunayahifadhi kwa sasa).
Kashfa
hiyo ya mtunga sheria huyo kupewa mimba na mheshimiwa mwenzake ambaye
ni mume wa mtu, ilipata mbeleko na kuifanya ivume zaidi, baada ya Mbunge
wa Mtera (CCM), Livingstone Lusinde, kulipuka bungeni:
“Humuhumu ndani
kuna wabunge wanawake wenye mimba zisizotarajiwa.”
Lusinde,
alitamka hayo Aprili, mwaka huu, wakati akichangia hotuba ya bajeti,
Ofisi ya Waziri Mkuu, kipindi ambacho bunge lilikuwa limechafuka
kutokana na wabunge kurushiana ‘mipasho’ wao kwa wao.
Kauli
ya Lusinde, pamoja na kupokelewa tofauti na wabunge wengi wanawake,
wakidai mheshimiwa mwenzao amewadhalilisha, upande mwingine, katika
‘vikao vya kwenye korido’, matukio ya vicheko na kugonga mikono
yalitawala na kunena kwa msisitizo “message delivered”, yaani ujumbe
umefika.
Wakati
mwandishi wetu akifuatilia sakata lenyewe, mbunge mwingine wa Viti
Maalum (CCM) ambaye jina lake tunaliweka kabatini, aliamua
kufunguka:
“Nashangazwa sana na haya madai, tunawasema wapinzani, wakati
hata kwetu (CCM) kuna watu wamepeana mimba.”
Mbunge
huyo alisema kuwa siyo siri mjengoni kuwa mmoja wa watunga sheria wa
CCM, anayetokea moja ya majimbo ya Kanda ya Magharibi, amempa ujauzito
mheshimiwa mwingine kutoka chama tawala, anayewakilisha viti maalum
(majina yao yamehifadhiwa kabatini kwa sasa).
Kwa
mujibu wa mtoa habari huyo, mbunge anayetajwa kupewa mimba, anatokea
kwenye ukoo wa mmoja wa vigogo waliowahi kushika nafasi za juu kabisa
kwenye Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Wabunge
mbalimbali waliozungumza na mwandishi wetu, walikiri kutambua uwepo wa
wenzao wenye uhusiano wa kimapenzi kiasi cha kufikia kupeana mimba.
Mbunge mwingine alithubutu kutamka: “Nini hao kupewa mimba na zinaonekana, wapo ambao wanapata na wanatoa. Yote hayo tunayajua.”
Katika
kufanyia kazi kila kinachozungumzwa, mwandishi wetu alizungumza na
baadhi ya wabunge ambapo Mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika,
alisema: Unajua madai ya mimba yanawahusu wanawake, kwa hiyo waulizwe
wenyewe.
“Kama umenitafuta mimi kwa kigezo kwamba ni mbunge kijana, basi waulize wabunge vijana wanawake,” alisema Mnyika.
Mbunge
wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila, alikiri kufahamu
kuwepo kwa tuhuma kwamba wapo wabunge wamepeana mimba lakini hawezi kuwa
na uhakika kwa sababu uhusiano wa kimapenzi ni jambo la faragha.
“Hayo
madai yapo, yanazungumzwa. Wapo wanaotajwa kuwa na uhusiano wa
kimapenzi, hayo ni mambo ya faragha. Sijui pengine walioanzisha haya
madai wana vipimo vyao,” alisema Kafulila.
Mbunge
wa Viti Maalum (CCM) Mkoa wa Morogoro, Sara Msafiri, alisema kuwa
haiwezekani wabunge kupata mimba zisizotarajiwa kwa sababu ni watu
wazima.
“Wabunge
tunapata mafunzo ya uzazi, kwa hiyo kama ni mimba basi mtu anakuwa
amepanga kuipata. Hakuna kitu kama hicho. Hata hilo la kutoa mimba
halipo kabisa, sijawahi kusikia mtu amefanya hivyo bungeni,” alisema
Sara.
Kwa
upande wa Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Grace Sindato Kiwelu,
alisema: “Sitegemei upande huo wa wabunge kupata mimba zisizotarajiwa,
kwani wanaofanya mapenzi ni watu wazima hivyo wanafanya wakijua kwamba
wanatarajia kupata nini.”
Mbunge
mwingine wa Viti Maalum (Chadema), Chiku Abwao, alisema: “Hakuna mbunge
anayepata mimba isiyotarajiwa, kwanza nilimshangaa mbunge kutamka mambo
kama hayo, alistahili kuwaambia watoto, lengo lake lilikuwa
kudhalilisha wanawake.”
Mbunge
wa Viti Maalum (CCM), Munde Tambwe, alisema: “Ile kauli ya Lusinde
kwamba kuna wabunge wanapata mimba zisizotarajiwa, nadhani kuna mtu
alikuwa anamlenga, kwa hiyo mimi siwezi kulizungumzia.”
No comments:
Post a Comment