Tuesday, April 9, 2013

Uhuru Kenyatta kuapishwa leo



 Rais Jakaya Kikwete na mkewe mama Salma Kikwete wakipokea maua mara baada ya kutua katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi kuhudhuria kuapishwa kwa Rais wa Nne wa Kenya Uhuru Kenyatta katika Uwanja wa Kasarani leo.

Maelfu ya wananchi wa Kenya tayari wamejaa uwanjani kusubiri kushuhudia tukio hilo la kihistoria.
Rais Jakaya Kikwete na mkewe mama Salma Kikwete na Balozi wa Tanzania nchini Kenya Dkt Batilda Burian wakipozi na wasichana waliowazawadia  mashada ya maua mara baada ya kutua katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Nne wa Kenya Uhuru Kenyatta. 
  Rais Jakaya Kikwete na mkewe mama Salma Kikwete wakilakiwa kwa heshima zote baada ya kutua katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi tayari kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Nne wa Kenya Uhuru Kenyatta na Makamu wake, William Ruto katika uwanja wa michezo wa Kasarani April 9, 2013

No comments:

Post a Comment