Monday, April 15, 2013

Mabaki ya ndege iliyomuua Bob Sambeke



Name:  DSC03435.JPG
Views: 0
Size:  7.26 MB

Mfanyabiashara maarufu katika mikoa ya Kilimanjaro na Arusha Joseph Sambeke (49) maarufu kama Bob Sambeke amekufa. 

Bob Sambeke alianguka na ndege ndogo juzi jioni kilomita moja kutoka Uwanja wa Ndege wa Arusha wakati akitoka mkoani Kilimanjaro.
 
Ndege ya Sambeke aina ya MT 7- namba 5H-QTT ilianguka saa 12.34 jioni baada ya bawa lake kugonga mti katika eneo la Magereza linalopakana na uwanja huo.

Alijeruhiwa na baadaye aliaga dunia akiwa njiani wakati akiwahishwa hospitalini na askari wa Magereza ambao wanaishi katika kambi alipoanguka. 

Mazishi yake yamepangwa kufanyika Alhamisi eneo la Karanga, Moshi.

Meneja wa Uwanja wa Ndege Arusha, Ester Dede amesema taarifa za awali zinaonyesha ndege hiyo ni mali ya marehemu Mawalla ambaye alikuwa mbia wa biashara na Bob Sambeki na imesajiliwa kupitia Kampuni ya Quality Tours & Travellers.

Wakili Alex Msando, ambaye pia alikuwa mshirika wa Mawalla, aliliambia gazeti hili kuwa Sambeke alikuwa ameinunua ndege hiyo kutoka kwa marehemu.
 
Dede alisema, ndege hiyo ikiongozwa na rubani Bob Sambeki ina uwezo wa kubeba watu wanne akiwamo rubani. Baadhi ya walioshuhudia tukio hilo, walisema kabla ya kuanguka ndege hiyo, ilikuwa ikiyumba na iligonga mti mkubwa katika moja ya mabawa yake na kupoteza mwelekeo.

Mmoja wa mashuhuda wa ajali hiyo, Julias Laizer alisema, aliona ndege hiyo ikigonga mti na kuyumba, kisha kudondoka chini na ndipo askari wa magereza walipojitokeza kutoa msaada. Laizer alisema Sambeki alikuwa peke yake na alijeruhiwa kichwani.

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgG6FIxSEQfc2LPY7BwcVUvOMie5ijhIkTmE2P6gfwow3GuH3bKWROVs8xTE6vBtJNEGDobVHkIrYY3rYakzU7tjURCxlnprUDZKRBEz-k_l6nnVVkCiixAO2FXeHf9hkoEZJ0hvIjZ060/s1600/ndege.jpg

No comments:

Post a Comment