Wanafunzi wa kike katika chuo kikuu cha Dodoma (UDOM) wanadaiwa
kufanya biashara ya ukahaba katika maeneo mbalimbali ya starehe mjini
Dodoma!
Inadaiwa kuwa wasichana hao wanauza miili yao kwa lengo la kujikimu kimaisha.
Tuhuma
hizo zimebainika wakati wa mahafali ya tatu ya UDOM huku takribani
wahitimu 6392 wakitunukiwa vyeti, stashahada, Shahada za kwanza, shahada za uzamili na
shahada za Uzamivu.
Kuna madai kwamba, wanafunzi hao huondoka chuoni usiku na kujiunga na wasichana wa mitaani waliokubuhu kwenye ukahaba maarufu kama
machangudoa.
Wakizungumza
na star tv wakati wa mahafali ya UDOM , baadhi ya wahitimu wamethibitisha
uwepo wa vitendo hivyo vilivyo kinyume na maadili.
Makamu Mkuu wa Chuo hicho Prof.Idris Kikula ametoa onyo kali kwa wote watakaobainika.
No comments:
Post a Comment