Monday, July 9, 2012

Mama Maria akabidhiwa tuzo ya heshima ya Baba wa Taifa


 Rais Dkt.Jakaya Kikwete akimkabidhi Mke wa Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere Tuzo ya Juu ya Heshima ya Taifa la Burundi aliyotunukiwa hayati Mwalimu Julius Nyerere wakati wa maadhimisho ya Miaka 50 ya Uhuru wa Burundi yaliyofanyika mjini Bujumbura wiki iliyopita.
 
Mwalimu Nyerere alitunukiwa tuzo hiyo kwa mchango wake wakati wa harakati za kupigania uhuru wa Burundi ambapo alikuwa mshauri wa karibu wa Waziri Mkuu wa Kwanza wa nchi hiyo Prince Louis Rwagasore. 
 
Rais Kikwete alimkabidhi Mama Maria tuzo hiyo leo asubuhi ikulu jijini Dar es Salaam. (Picha Freddy Maro).

No comments:

Post a Comment