Wananchi wakisaidia uokoaji katika eneo la ajali
Picha zikionyesha ajali iliyoyahusisha basi dogo aina ya Toyota Coaster na lori la mizigo iliyotokea katika Kijiji cha Ntangano, Ijombe Mbeya Vijijini barabara ya Mbeya- Kyela.
WATU
13 wamekufa na wengine kadhaa kujeruhiwa katika ajali
iliyohusisha magari mawili eneo la Ntangano Ijombe Mbeya Vijijini
barabara ya Mbeya Kyela.
Ajali
hiyo imelihusisha lori lenye namba T.658 ASJ lililokuwa na tela namba
T.150 ASN iliyokuwa ikitokea mpakani mwa Tanzania na Malawi (Kasumulo)
pamoja na Toyota Coaster yenye namba T.886 BDZ iliyokuwa ikitoka Jijini Mbeya
kuelekea Wilayani Kyela.
Wananchi waliofika Hospitali ya Rufaa Mbeya kutazama miili ya marehemu
Miili ya marehemu ikipelekwa katika Hospitali ya Rufaa Mbeya
Wafanyakazi wakiwawahisha majeruhi kupata huduma ya kwanza.
Picha kwa hisani ya www.mbeyayetu.blogspot.com na www.francisdande.blogspot.com
Picha kwa hisani ya www.mbeyayetu.blogspot.com na www.francisdande.blogspot.com
No comments:
Post a Comment