Katibu
Mkuu wa Chama cha Demokrasa na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa
(kulia), akizungumza baada ya kufungua moja ya matawi mjini Newala
ikiwa ni sehemu ya ziara ya viongozi wa chama hicho. Katikati ni
Mwenyekiti, Freeman Mbowe akiwa amembeba mtoto Muaza Mohamed na kushoto
ni Mkamu Mwenyekiti, Zanzibar, Ali Issa Mohamed.
Akinamama
wa kijiji cha Mbuyuni, katika jimbo la Lulindi mkoani Mtwara, wakiimba
nyimbo za kumpongeza Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo
(CHADEMA), Freema Mbowe, mara baada ya mkutano wake wa hadhara katika
kijiji hicho
Akinamama
wa kijiji cha Mbuyuni katika jimbo la Lulindi mkoani Mtwara,
wakiitikia kibwagizo cha Peoples Power kinachotumiwa na Chama cha
Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), wakati wa mkutano wa Mweneykiti wa
chama hicho, Freeman Mbowe
Mbunge
wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika (CHADEMA), akihutubia mkutano wa
hadhara wachama hicho, wa Kampeni ya Vua Gamba Vaa Gwanda, uliofanyika
mjini Tandahima mkoani Mtwar.
Mwenyekiti
wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe
akihutubia mkutano wa hadhara wa Oparesheni Vua Gamba Vaa Gwanda,
katika mji wa Chiungutwa jimbo la Lulindi mkoani Mtwara
Mwenyekiti
wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe
akipandisha bendera ya chama hicho, wakati alipofungua Tawi jipya
katika Mtaa wa Mkombozi mjini Newala. Kushoto kwake ni Katibu Mkuu wa chama
hicho, Dk. Willibrod Slaa na kulia kwake ni Makamu Mwenyekiti, Zanzibar,
Ali Issa Mohamed.
Picha zote na www.francisdande.blogspot.com
No comments:
Post a Comment