Monday, April 27, 2009

Ni Arsenal na Man United Jumatano

Mashine za Arsenal. Arshavin na Fabregas



Cesc Fabregas akishangilia bao alilofunga jana, alicheka na nyavu mara mbili





Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger

KOCHA wa Arsenal ya Uingereza, Arsene Wenger amesema The Gunners wana uwezo wa kuifunga timu yoyote duniani.


Wenger amesema, haidharau Man United lakini anakwenda Old Trafford kushinda.


Kocha huyo Mfaransa amesema, ingawa Mashetani wekundu wana uzoefu, pasi za vijana wake si mchezo hivyo wanakwenda kutafuta goli na kushinda.

Vinara hao wa soka Uingereza watapambana Jumatano katika kipute cha nusu fainali ligi ya mabingwa barani Ulaya.

Jana Arsenal waliinyuka Middlesbrough mabao 2 kwa bila, Juzi Man U iliishinda Totenham Hotspurs 5 kwa 2.
Sindano mpya ya The Gunners, Andre Arshavin haitacheza game la keshokutwa.

No comments:

Post a Comment