Wednesday, March 4, 2009

Mke wa Rais afungwa jela



MKE wa Rais wa Zambia, Frederick Chiluba, Regina, amehukumiwa kifungo cha miaka mitatu na nusu jela baada ya kupatikana na makosa ya rushwa na wizi wa fedha za umma.

Alipatikana na hatia ya kupokea fedha zilizoibwa serikalini wakati Chiluba alipokuwa madarakani, akanunua nyumba tatu alizofanyia biashara.

Regina pia alishindwa kuieleza mahakama alipataje dola za Marekani 100,000 zilizokutwa katika akaunti yake.

Miongoni mwa sifa za Regina ni urembo, na 'hupiga pamba' za gharama.

No comments:

Post a Comment