Monday, June 11, 2012

Msiba Kenya



The scene where the Police Helicopter crashed in Ngong forest.
http://africanspotlight.com/wp-content/uploads/2012/06/crashinpics6100612.jpg
http://news.bajansunonline.com/wp-content/uploads/2012/06/60809634_jex_1430951_de27-1.jpg

 WAKENYA wameanza siku tatu za maombolezo baada ya kifo cha Waziri wa Usalama wa Kenya, Profesa George Saitoti, na naibu wake, Orwa Ojode.

Viongozi hao walikufa jana asubuhi  kwenye ajali ya helikopta ya polisi katika eneo la Ngong, nje ya Nairobi.

Rais wa Kenya, Mwai Kibaki amesema, kifo cha Bwana Saitoti ni msiba mkubwa kwa taifa, na serikali imetangaza kuwa baraza la mawaziri linakutana leo Jumatatu, kujadili tukio hilo.

"Ndege hiyo ya aina ya Eurocopter ya police airwing, ambayo ilikuwa inaelekea Yugis, ilikuwa imembeba Waziri George Saitoti, naibu waziri Orwa Ojode na maafisa rubani wa ndege, Nancy Gitwanja na Luke Oyugi, na vilevile askari wawili ambao wanakuwa wanaandamana na Waziri Saitoti, Inspector Tonkei na Thomas Murimi"


  Saitoti aliwahi kuwa Makamu wa Rais na Waziri wa fedha katika serikali ya Rais Moi,.

Abiria wote sita, wakiwemo marubani wawili na walinzi wa mawaziri hao waliokuwa kwenye helikopta hiyo wamekufa.

Miili ya marehemu wote imeteketezwa kabisa na haitambuliki na hadi sasa chanzo cha ajali hiyo hakijafahamika.



Mawaziri hao wawili walikuwa wakielekea jimbo ambalo Orwa Ojode analiwakilisha bungeni la Ndhiwa, katika shughuli ya Harambee kulichangia kanisa moja huko.


Saitoti alikuwa miongoni mwa wanasiasa mashuhuri nchini Kenya waliokuwa wakipania kugombea kiti cha urais katika uchaguzi mkuu ujao.

Walioshuhudia ajali hiyo wamesema waliona helikota hiyo ikizunguka angani kabla ya kuanguka katika msitu wa Ngong.

No comments:

Post a Comment