Tuesday, May 22, 2012

Wakuu wa mikoa na wilaya wafundwa Dodoma


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Hawa Ghasia (kushoto) na Waziri wa zamani na mwanasiasa mkongwe, Kingunge Ngombale Mwiru katika Kikao cha Wakuu wa Mikoa na Wilaya pamoja na Makatibu Tawala wa Mikoa kwenye Kituo cha mikutano cha St. Gaspar Mjini Dodoma.

Waziri wa zamani na Mwanasiasa mkongwe Kingunge Ngombale Mwiru akitoa mada katika Kikao cha Wakuu wa Mikoa na Wilaya  na  Makatibu Tawala wa Mikoa kwenye Kituo cha Mikutano cha St.Gaspar Mjini Dodoma.


Baadhi ya washiriki wa Semina ya Wakuu wa Mikoa na Wilaya pamoja  na Makatibu Tawala wa Mikoa wakimsikiliza Waziri Mkuu, Mizengo Pinda wakati alipofungua kikao chao  kwenye Kituo cha Mikutano cha St. Gaspar Mjini Dodoma.(Picha zote na Ofisi ya Waziri Mkuu).
WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda amewataka wakuu wa mikoa na wilaya nchini kujiheshimu na kuacha kujiona miungu watu.
Pinda pia amewataka viongozi hao wa Serikali kutokuwa walevi na wahuni.
Amewataka wawe kimbilio la wanyonge kwa kutenga nafasi za kusikiliza kero za wananchi katika mikoa na wilaya wanazoongoza.


Aliwataka kuacha kufikiria kujinufaisha wao kwanza na kuwasihi wakiona malalamiko na kero za wananchi zinafikishwa kwa Rais, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu, ni dhahiri kuwa viongozi hao hawatimizi wajibu wao. 

"Haipendezi kwenda kwenye baa ya wazi, kabia kakikukolea unatoka pale ukitaka usindikizwe… watu pale wamekuona sijui uko na mke au mume wa mtu; mnatakiwa kuwa na mipaka, kunywa kabia kako jiheshimu, hata kama unataka kudondoka basi dondoka kwa heshima," alisema.


"Mnatazamiwa kuonesha njia, nini kifanyike ili kukabiliana na changamoto na malalamiko ya wananchi, mnatakiwa kuyapatia ufumbuzi matatizo yanayowakabili badala ya kuwa sehemu ya matatizo hayo na ili kufanikisha, kila mmoja atambue na akubali kuwa uongozi ni kufanya kazi zaidi," alisema.


No comments:

Post a Comment