Monday, March 23, 2009

Nyota Big Brother aaga dunia


Mwil wa jade ukitolewa nyumbani kweke kwenda kuhifadhiwa


Mama mzazi wa Jade, Jackiey wakati mwiili wa mwanae ukitolewa ndani kwenda kuhifadhiwa

Jade na tuzo yake

Jade baada ya madaktari kumueleza ana kansa ya kizazi

Jade akiaga mashabiki wake wakati akitoka hotelini baada ya kufunga ndoa Februari mwaka huu

Jade akiwa hospitali

Watoto wa Jade, Bobby(5) na Freddie(4)


NYOTA wa Big Brother na vipindi halisi vya televisheni Uingereza, Jade Goody(27) amefariki dunia akiwa usingizini nyumbani kwake, Upshire Essex nchini humo.

Bila shaka kifo hiki kimewasikitisha wengi nikiwamo mimi kutokana na yale aliyoyafanya katika siku za uhai wake.

Agosti mwaka jana madaktari waligundua kuwa, TV Star huyo alikuwa akisumbuliwa na kansa ya kizazi iliyosambaa kwenye sehemu nyingine za mwili.

Kabla ya kuaga dunia jana asubuhi, alikuwa akipoteza fahamu mara kwa mara na alikuwa kwenye maumivu makali.

Jade alifahamu kuwa hakuwa na siku nyingi za kuishi hivyo alifanya mambo kadhaa yatakayobaki katika kumbukumbu za wengi ikiwa ni pamoja na kuingia mikataba na majarida na vituo vya televisheni ili apate fedha za kuwaachia wanawe, Bobby(5) na Freddie(4).

Watu wengi Uingereza, Ulaya na mabara mengine wamekuwa wakifuatilia taarifa za msichana huyo aliyepambana hadi dakika za mwisho.

Huku akiumwa na akifahamu kuwa ana asiku chache za kuishi, Februari 22 mwaka huu Jade alipanda madhabahuni kufunga ndoa na Jack Tweed, walilala pamoja usiku mmoja tu.

Alihakikisha kuwa kabla ya kuiaga dunia wanawe wanabatizwa, walipata huduma hiyo ya kiroho Machi saba mwaka huu, Machi 11 akajiruhusu kutoka hospitali akaenda nyumbani kwake kukisubiri kifo.

Mungu ailaze Roho ya Jade mahala pema peponi, amen.

No comments:

Post a Comment