Monday, March 23, 2009

Hoteli Bagamoyo zateketea kwa moto

HABARI nilizozipata hivi punde zinadai kuwa hoteli kadhaa katika ufukwe wa bahari ya Hindi wilayani Bagamoyo, Pwani zimeteketea kwa moto.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, moto bado unaendeelea kusambaa kwenye hoteli nyingine na juhudi za kuuzima zinaendelea.

Hoteli nyingi kwenye eneo hilo zimejengwa kwa makuti hivyo ni rahisi kushika moto.

Miaka michache iliyopita sehemu ya hoteli ya Sea Cliff, Dar es Salaam iliungua kwa moto.

No comments:

Post a Comment