Monday, March 23, 2009

Moto wateketeza hoteli mbili Bagamoyo


HOTELI mbili za kitalii wilayani Bagamoyo, Pwani zimeteketea kwa moto leo asubuhi.

Kwa mujibu wa polisi, moto huo umeteketeza Oceanic Bay Resort, na Paradise Beach Resort.

Moto huo ulianzia katika jiko la hoteli ya Paradise na ukasambaa hadi katika hoteli ya Oceanic.

Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Serengo mrengo sehemu kubwa ya mali za wateja zimeokolewa, ila mali za wamiliki nyingi zimeteketea.

Uongozi wa Hoteli ya Paradise umeahidi kuwa kesho utazungumza na waandishi wa habari ili kueleza kwa undani kuhusu ajali hiyo.

No comments:

Post a Comment