Wednesday, March 25, 2009

Jade kuzikwa na gauni la harusi


Jade akiaga mashabiki wake wakati akitoka hotelini kurudi hospitali Februari 23 mwaka huu baada ya kufunga ndoa na Jack Tweed Februari 22.

Ilikuwa ni mara ya mwisho kwake kuonekana hadharani, alifariki dunia akiwa usingizini nyumbani kwake, Upshire, Essex nchini Uingereza.


Watoto wa Jade, Freddie(kushoto) na kaka yake, Bobby

Jade na Jack wakiapa kuwa mume na mke, Februari 22 mwaka huu.


Jade siku ya harusi yake Februari mwaka huu

NYOTA wa Big Brother Uingereza, Jade Goody atazikwa Aprili nne mwaka huu akiwa amevishwa gauni alilovaa siku alipofunga ndoa na Jack Tweed Februari 22 mwaka huu.

Kabla ya kuaga dunia Machi 22 mwaka huu, mtangazami huyo nyota kipindi halisi vya televisheni aliacha usia kwamba azikwe na gauni hilo na pete yake yake ya ndoa.

Jade pia alichagua picha ya wanawe, Bobby(5) na Freddie(4) hivyo itawekwa ndani ya jeneza lake.

Taarifa za kifo chake zimetawala vyombo vingi vya habar vya kimataifa na huenda mamilioni watashuhudia mazishi yake.

No comments:

Post a Comment