Friday, June 8, 2012

Rais Kikwete aapisha majaji

Rais Jakaya Kikwete akimwapisha Semistocles Kaijage (kulia) kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania leo jijini Dar es Salaam. 
 
Kabla ya uteuzi huo Semistocles Kaijage alikuwa jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam.
Rais Jakaya Kikwete akifurahia Jambo na kamishna wa Tume ya Utumishi wa Mahakama Edward Rutakangwa (wa tatu kutoka kushoto)  mara baada ya kumwapisha leo Ikulu jijini Dar es Salaam. 
 
Wengine kutoka kushoto ni Jaji wa mahakama ya Rufani Mussa Kipenka na Jaji  Semistocles Kaijage (wa kwanza kushoto).
  Jaji Mussa Kipenka akipongezwa na baadhi ya ndugu waliohudhuria hafla fupi ya kuapishwa kwake kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete akimwapisha Edward Rutakangwa kuwa kamishna  wa Tume ya Utumishi wa Mahakama katika hafla fupi iliyofanyika leo Ikulu jijini Dares Salaam.
Jaji wa mahakama ya Rufaa Semistocles Kaijage akizungumza na vyombo vya habari mara baada ya kuapishwa leo Ikulu jijini Dar es Salaam. 
 
Jaji wamahakama ya Rufani , Mussa Kipenka akisaini hati ya kiapo mara baada ya kuapishwa na Rais  Dkt. Jakaya kikwete leo Ikulu jijini Dar es Salaam. 
 
Anayeshuhudia ni jaji mkuu wa Tanzania Mohammed Chande Othman.

No comments:

Post a Comment