WAZIRI mpya wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki,
ameshtushwa na ubadhirifu wa kutisha katika wizara
hiyo, hususani Idara ya Wanyamapori unaodaiwa kufanywa na baadhi ya watendaji
wake.
Waziri Kagasheki amewaeleza waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuwa, idara hiyo inanuka kwa uozo
unaotokana na wizi na ubadhirifu mkubwa ambao umeleta hasara kwa taifa.
Aliyasema hayo baada ya kuzindua Bodi ya
Ushauri ya Wizara ya Wakala wa Huduma za Misitu (TFS) jijini Dar es
Salaam, jana
Kagasheki alidai Idara ya Wanyamapori inaongoza kwa madudu ya kutisha katika wizara hiyo na kwamba, fedha
zilizotafunwa na wajanja hao ni nyingi.
“Jamani Idara ya Wanyamapori ina fedha nyingi, lakini zinaliwa na watu
kwa maslahi binafsi, na kama fedha hizo zingekuwa zinapelekwa
serikalini kama inavyohitajika, nchi hii kwa sasa ingefika mbali, mimi
naogopa hata kutaja kiasi cha fedha hapa hadharani,” alisema.
Balozi Kagasheki amesema , usafirishaji
wanyamapori nje ni mkubwa mno licha ya serikali kusitisha biashara hiyo.
Alisema , biashara ya kusafirisha
wanyama pori inafanywa kati ya wafanyabiashara wa ndani na baadhi ya
watendaji, ambao hawajali na wanaonekana kutumia kila mbinu
kuifanikisha.
Balozi Kagasheki alionesha hofu
yake ya kukabiliana na wafanyabiashara na baadhi ya maafisa wa wizara
hiyo,na ameomba msaada kutoka taasisi nyingine, vikiwemo vyombo
vya habari kusaidia kupambana na ‘genge’ la wabadhirifu hao.
“Katika idara kunahitaji usaidizi maana hapa ni vita, na hata ninyi
waandishi nafikiri mnaweza tukasaidiana kwa kuwa najua mtakuwa mnawajua
sana wafujaji. Kuwaondoa hawa ni kutangaza vita,” alisema.
Amesema, atavunja uongozi wa idara hiyo na
kuiunda upya haraka.
Alisema ataagiza kufanyika kwa sensa kwa wanyama na kuweka wazi kila kitu, ili kunusuru kumalizika kwa wanyama wote.
“Tutawajulisha wananchi waelewe, hatutachelewa maana watu wameshajua,
wasije kuwamalizia wanyama wote,” alisema Balozi Kagasheki.
|
No comments:
Post a Comment