Wabunge kutoka Kambi ya upinzani jana walimsuta Mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe baada ya Mbunge huyo kumweleza Mbunge wa Nyamagana, Ezekiah Wenje kuwa alikosa ustaarabu kwa kutomtii Mwenyekiti wa Bunge, Sylvester Mabumba.
Mabumba alimuamuru Wenje atoke nje ya ukumbi wa Bunge baada ya Mbunge huyo kusimama na kutaka kuzungumza jambo alilosema ni la dharura bila ruksa ya Mwenyekiti wa Kikao.
Baada ya Filikunjombe kusema Wenje hakuwa mstaarabu, wabunge walimvaa, wakashutumu na kumsuta kuwa alikosa uzalendo kwa kuwa mwenzake alitaka kuzungumzia jambo la msingi linalogusa afya za wananchi.
Kwa mujibu wa Wenje, Kanuni za Bunge zinamruhusu Mbunge kuzungumzia jambo la dharura, na kwamba, yeye alitaka kuomba Bunge lijadili suala la samaki wanaodaiwa kuwa na sumu walioingizwa nchini kutoka nchini Japan.
No comments:
Post a Comment