Monday, March 30, 2009

Watoto wa Jade kutohudhuria mazishi


Jade, Jack, na watoto wa Jade, Freddie(Kushoto) na Bobby siku ya harusi Februari 22 mwaka huu

Jeff Braizer na Jade wakiwa na mtoto wao wa kwanza, Bobby

Jade akiwa na mwanae wa kwanza, Bobby baada ya kutoka katika jumba la Big Brother

Jade wakati akiumwa saratani ya kizazi

WATOTO wa Mtangazaji nyota wa vipindi halisi vya televisheni, Jade Goody(27) hawatahudhuria mazishi ya mama yao mzazi Jumamosi wiki hii.

Baba yao mzazi, Jeff Brazier(29) na bibi yao mzaa mama, Jackiey Budden(50) wameamua hivyo kwa maelezo kwamba Bobby(5) na Freddie(4) ni wadogo sana kuweza kustahimili kuona mama yao akizikwa.

Wamesema, kama watashuhudia mama yao akizikwa watabaki na kumbukumbu mbaya kuhusu mama yao hivyo hawatakwenda makaburini.
Jade alifariki dunia Machi 22 nyumbani kwake, aliugua saratani ya kizazi.

No comments:

Post a Comment