Thursday, March 26, 2009

Mume kuiomba msamaha maiti


Mume wa Jade Goody, Jack Tweed jana

Jade na Jack wakifunga ndoa Februari 22 mwaka huu

Jade na Jack walipokuwa boyfriend na girlfriend

Mama mzazi wa Jade akiwa na ua waliloacha mashabiki wa Jade nje ya nyumba yake(Jade)


MUME wa mtagazaji nyota wa vipindi halisi vya televisheni, Jade Goody(27) anapanga kwenda kuuona mwili wa marehemu mkewe ili amuombe msamaha na kumueleza kuwa anampenda.

Jack Tweed(21) anapanga kufanya hivyo kwa kuwa anajihisi ni mkosefu hivyo anapanga kutumias nafasi hiyo kumuomba Jade msmaha.

Jack amekuwa ni mtu wa majonzi tangu Jade afariki dunia Machi 22, na kila mara anabubujikwa na machozi.

Jack na Jade walifunga ndoa Februari 22, wamekuwa mke na mume kwa mwezi mmoja tu, na walilala pamoja usiku mmoja tu hotelini baada ya harusi yao.

Jade anatarajiwa kuzikwa Aprili nne, ameacha watoto wawili, Bobby(5) na Freddie(4)

1 comment: