Monday, March 30, 2009

Ghorofa lanusurika kuungua Dar es Salaam

JENGO la ghorofa linalomilikiwa na Msajili wa Nyumba(NHC) kitalu namba 1285/84 jijini Dar es Salaam limenusurika kuungua usiku wa kuamkia leo.

Eneo la mgahawa katika jengo hilo Mtaa wa Zaramo imeungua, pembeni ya eneo sehemu hiyo kuna duka la nyama na chumba za biashara ya chips na kuku wa kupaka inayofanywa usiku.

Mashuhuda wamesema, moto huo ulizimwa kwa ushirikiano wa wananchi na magari ya zimamoto.

Sehemu ya juu ya jengo hilo linalotazamana na ofisi za DTV/ Channel Ten wanaishi wanafunzi wanaosoma katika vyuo mbalimbali jijini Dar es Dalaam

No comments:

Post a Comment