Monday, September 23, 2013

Kazi ya kuokoa mateka Nairobi inaendelea

Serikali ya Kenya imesema, vikosi vya uokoaji vimeua magaidi mawili na vimeokoa takribani mateka wote waliokuwa wametekwa na magaidi katika jengo la maduka la Westgate jijini Nairobi tangu Jumamosi mchana.nullWaziri wa Mambo ya Ndani nchini Kenya, Joseph ole Lenku amesema, kazi ya kuokoa mateka katika jengo hilo karibu inakwisha.

Amewaeleza waandishi wa habari kwamba, magaidi wote ni wanaume, lakini baadhi yao wamevaa nguo za kike, na kwamba, wanakadiriwa kuwa kati ya 10 hadi 15.
Kwa mujibu wa kiongozi huyo, waokoaji wamewazingira magaidi waliojificha kwenye maduka yaliyopo kwenye jengo hilo kubwa na watawasambaratisha.

Kwa mujibu wa Waziri Lenku, hadi sasa magaidi wawili wameuawa, wenzao wamejeruhiwa, na kwamba, askari 10 wamejeruhiwa katika mapambano na magaidi hao.
Amesema, moshi unaotoka kwenye jengo hilo unatokana na kitendo cha magaidi hao kuchoma magodoro ili kuharibu mipango ya wanajeshi kuokoa mateka.

No comments:

Post a Comment