Wachezaji Haruna Niyonzima wa Yanga (kushoto) na Uhuru Selemani wa Simba
wakiwa na majonzi baada ya kuuona mwili wa Mafisango katika Hospitali ya Muhimbili, Dar es Salaam.
Mchezaji huyo 'kiraka', ameaga dunia muda mfupi baada ya kupata ajali ya gari katika eneo la Tazara.
Mafisango alikuwa na uwezo wa kucheza namba 6, 8, 10 na hata 11.
Kwa
mujibu wa Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage, Mafisango alipata
ajali hiyo wakati akiendesha gari, na kwamba, alikuwa anamkwepa
mwendesha pikipiki.
Rage amesema, wakati anamkweka
mwendesha pikipiki, gari hilo liliingia mtaroni, mchezaji huyo raia wa
Rwanda akaumia sana, na aliaga dunia muda mfupi baadaye.
Amesema, Mafisango alikuwa na rafiki yake, na mtu mwingine, na kwamba, wameumia.
Mafisango ameaga dunia siku chache baada ya kocha wa timu ta taifa ya Rwanda kumuita katika timu ya taifa ya nchi hiyo.
Mbunge wa jimbo la Korogwe CCM Steven Ngonyani Prof Maji Marefu
akizungumza na wanahabari hospitalini hapo kuelezea masikitiko yake kuhusu kifo cha mchezaji huyo.
Haruna Moshi akitoka kwenye chumba cha kuhifadhia maiti huku akilia kwa
uchungu baada ya kuhakikisha kweli mwenzao Patrick Mafisango ameaga dunia.
Mchezaji wa zamani wa Simba Boniface Pawasa akilia kwa uchungu huku
akifarijiwa na Mchezaji Uhuru Selemani.
Pawasa amesema jana
walikuwa naye kwenye muziki katika klabu ya Maisha Oysterbay wakati
bendi ya Akudo Impact ikifanya onyesho klabuni hapo na marehemu alimuaga
kwamba anaenda nyumbani baadae akapigiwa simu kwa simu ya marehemu
akiambiwa mwenye simu hii amefariki dunia kwa ajali.
Uongozi wa Simba umesema, unawasiliana na Ubalozi wa Rwanda na mashirika ya ndege ili kukamilisha utaratibu wa vibali mbalimbali tayari kwa kuusafirisha mwili wa marehemu kwenda nchini Rwanda kwa mazishi na taarifa kamili ya lini utasafirishwa itatolewa kesho mara baada ya kukamilika kwa taratibu zote.
Aliyewahi kuwa mchezaji wa timu ya Simba Mrundi Ramadhana Wasso
akihojiwa na waandishi wa habari kuelezea masikitiko yake kutokana na
msiba huo.
(Picha kwa hisani ya blog ya Fullshangwe).
No comments:
Post a Comment